Monday, March 2, 2015

Mkuu wa Polisi wilaya ya Arusha Mrakibu wa Polisi (SP) Jumanne Muliro akitoa elimu ya Polisi Jamii kwa vikundi vya Ulinzi Shirikishi ili viweze kufanya kazi kwa weledi.(Picha na Rashid Nchimbi wa Jeshi la Polisi Arusha)

\Na Mahmoud Ahmad Arusha
Mkuu wa Polisi wilaya ya Arusha MrakibuwaPolisi (SP) Jumanne Muliro amevitaka vikundi vya ulinzi shirikishi pindi wanapokuwa katika kazi za doria kutowabughudhi wananchi badala yake wanatakiwa kufanya kazi zao kwa kufuata sheria.

Alisema utendaji bora wa kazi kwa kuzingatia nidhamu na sheria utaongeza imani kwa wananchi hali ambayo itawafanya wajitolee na kuendelea kuvichangia vikundi hivyo hatimaye kuboresha maslahi yao wenyewe na vikundi hivyo kwa ujumla kwa maana ya vifaa.

 “Hakuna sheria inayomkataza mtu yoyote kutembea usiku lakini pia ni jukumu lenu nyinyi askari kumhoji yeyote mtakayekutana naye usiku kwa kutumia taaluma mlionayo nayo ili kuweza kubaini ukweli” Alifafanua Mkuu huyo wa Polisi.

No comments:

ENGEZA HAMU YA CHAKULA MAMII PILI PILI

Zipo katika ubora wa 100% nitamu na yenye laza nzuri