Friday, February 27, 2015

Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Morrice Oyuke (Kulia)akitoa taarifa ya Pato la Taifa kwa kipindi cha robo tatu ya mwaka 2014 leo jiji Dar es salaam. Pato hilo kwa mwaka 2014 limefikia kiasi shilingi trilioni 21.2  kutoka trilioni 19.8 za mwaka 2013, Kushoto ni  Mtakwimu Mkuu wa Ofisi hiyo Bw. Gregory Milinga,

Aron Msigwa –MAELEZO.
Pato la Taifa (GDP)  katika kipindi cha robo ya tatu ya mwaka 2014 limeongezeka hadi kufikia shilingi trilioni 21.2 kutoka shilingi trilioni 19.8  za kipindi kama hicho kwa mwaka 2013.

Akizungumza na waandishi wa habari leo jiji Dar es salaam, Mkurugenzi wa Takwimu za Uchumi wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu (NBS) Bw. Morrice Oyuke, amesema kuwa katika kipindi cha robo tatu ya mwaka 2014 sekta nyingi za uchumi zimefanya vizuri katika uzalishaji ikilinganishwa na mwaka 2013. 

Amesema katika kipindi hicho shughuli za uchimbaji wa Madini , Mawe na Kokoto zimekua kwa asilimia 5.2 ikilinganishwa na asilimia 3.3 za mwaka 2013, Uzalishaji wa bidhaa za viwandani  ukikua kwa asilimia 10.8 kutoka asilimia 10.4 pamoja na ongezeko la uzalishaji wa umeme kwa asilimia 10.7 kutoka asilimia 10.3 za mwaka 2013 kutokana na matumizi ya mafuta na Gesi.

Amezitaja sekta nyingine kuwa ni usambazaji maji ambao umekua kwa asilimia 12.7 kutoka 6.9 za mwaka 2013, Habari na Mawasiliano kwa asilimia 11.9 kutoka 7.0, Shughuli za Fedha na Bima zikikua hadi kufikia asilimia 13.9 kutoka asilimia 6.8 za mwaka 2013.

Ameongeza  kuwa  katika kipindi hicho huduma za upangishaji wa nyumba zilikua hadi kufikia asilimia  2.2 kutoka 2.1, shughuli za kitaalamu, kisayansi, ufundi na utawala  zikifikia  asilimia 5.4 kutoka asilimia 1.0 ya mwaka 2013.

 Bw. Oyuke amezitaja  shughuli  nyingine kuwa ni uendeshaji wa Serikali ambazo zilikua  kwa asilimia 4.9 ikilinganishwa na 4.4, huduma za Elimu kwa asilimia 3.7 kutoka 3.5, Afya kwa asilimia 8.1 pamoja na shughuli za Sanaa na Michezo ambazo zilikua kwa asilimia 2.5 ikilinganishwa na 1.6 ya mwaka 2013.

Aidha, amebainisha kuwa uzalishaji wa Almasi katika kipindi cha robo tatu ya mwaka 2014 ulikuwa karatasi 66,508 ikilinganishwa na karatsi 27,828 zilizozalishwa katika kipindi kama hicho mwaka 2013

No comments:

ENGEZA HAMU YA CHAKULA MAMII PILI PILI

Zipo katika ubora wa 100% nitamu na yenye laza nzuri